Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) amesema kuwa moja ya jambo ambalo nchi inalihitaji kwa sasa ni kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati na makundi maalumu katika ununuzi wa umma ili washiriki katika shughuli za kiuchumi na kuwa walipakodi wakubwa.
Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, akimkabidhi mwakilishi wa wazee, mwongozo wa kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati na makundi maalumu katika ununuzi wa umma, jijini Dodoma.
Dkt. Nchemba amesema hayo jijini Dodoma wakati wa hafla ya utiaji saini wa Hati ya Makubaliano kati ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC) na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati na makundi maalumu katika ununuzi wa umma, ambapo Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, alikuwa mgeni rasmi.
Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, akiteta jambo na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakati wa hafla ya kusainiwa kwa Hati ya makubaliano ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati na makundi maalumu katika ununuzi wa umma, jijini Dodoma.
“Kama kwenye nchi tutakuwa na watu hawashiriki katika shughuli za uzalishaji na Uchumi ni itakuwa vigumu sana kutengeneza walipakodi wakubwa”, alisema, Dkt. Nchemba.
Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Doto Biteko, akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Jenista Mhagama, Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), Menejimenti ya Wizara ya Fedha na viongozi wengine baada ya kusainiwa kwa Hati ya makubaliano ya uwezeshaji katika ununuzi wa umma, jijini Dodoma.
Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, wakifurahia jambo na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakati wa hafla ya kusainiwa kwa Hati ya makubaliano ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati na makundi maalumu katika Ununuzi wa umma, jijini Dodoma.
Alisema wazo hilo la kuwawezesha katika ununuzi wa umma, kwa upande wa Wizara ya Fedha linaepusha kukimbizana na watu masikini kutafuta kodi hivyo kusaidia kukusanya kodi kwa watu ambao wanashiriki katika shughuli za kiuchumi na wanauwezo, jambo ambalo ni faida.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, akimkabidhi Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), mwongozo wa kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati na makundi maalumu katika ununuzi wa umma, jijini Dodoma.
Dkt. Nchemba amemshukuru Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, kwa kukubali kushiriki katika hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo na kwamba baada ya zoezi hilo anaamini utekelezaji wa mawazo yaliyowekwa yatatekelezwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Eliakim Maswi (kushoto) na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC), Bi. Beng’i Issa, wakisaini Hati ya makubaliano ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wa kati na makundi maalumu katika ununuzi wa umma, wakishuhudiwa na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Mhe. Doto Biteko, jijini Dodoma.
Aidha amezipongeza timu za wataalamu kwa kazi nzuri waliyofanya iliyosababisha kusainiwa kwa makubaliano hayo ambayo yataziba mapungufu yaliyokuwa yanajitokeza hususani kwenye eneo la utekelezaji kwa kuwa kuna mambo yalikuwa kwenye maandishi lakini utekelezaji ulikuwa unakosekana..