_Asema Serikali itaendelea kuongeza fedha za mikopo ya elimu ya juu_

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amezitaka taasisi za elimu nchini kutowazuia wanafunzi kufanya mitihani ya masomo yao kwa kushindwa kulipa ada.

Pia, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuongeza fedha za mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na vyuo vya kati ili wanafunzi wengi zaidi wanufaike na mikopo hiyo.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa maelekezo hayo leo (Alhamisi Mei 14, 2026) Bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Latifa Khamis Juwakali aliyetaka kujua mkakati wa Serikali kiuhusu wanafunzi wanaozuiwa kufanya mitihani kwa kutokulipa ada.

Share Story

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *