80917316-d525-4a6e-8ad2-50c86826b2d2

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkataba wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Barabara ya Kitusha–Kinampanda–Kisana–Kisiriri umeshasainiwa, hatua inayofungua njia ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo unaotarajiwa kubadilisha shughuli za usafiri na uchumi katika maeneo ya Wilaya ya Iramba.

Dkt. Mwigulu amesema hayo leo, Jumapili Juni 14, 2026, wakati akizungumza, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Tarafa ya Kinampanda katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Kinampanda, Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Amesema Serikali imekamilisha hatua muhimu ya upatikanaji wa fedha za mradi huo na kwamba changamoto iliyobaki sasa ni kukamilisha taratibu za kumpata mkandarasi atakayetekeleza ujenzi huo.

“Leo tunavyoongea, mkataba wa upatikanaji wa fedha umeshasainiwa. Kwa hiyo fedha si tatizo tena. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Halmashauri ambao walishuhudia kusainiwa kwa mkataba huo,” amesema Dkt. Mwigulu.

Share Story

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *