
Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Julai 20, 2026 amekutana na viongozi wa Benki ya CRDB katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Oysterbay, jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo hayo, wamejadili masuala mbalimbali yenye lengo la kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Benki hiyo katika kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya Taifa.